***

***

Technology

Star wa Soka Tanzania Mbwana Samatta akabidhiwa demu wa kighana....





Binti huyo pamoja na nguli wa televisheni ya SuperSport, Robert Marawa ndiyo watakaokabidhiwa jina la staa wa Tanzania, Mbwana Samatta kwenye tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika leo Alhamisi na kumtangaza kama atashinda tuzo.

Kama ni Mtazamaji Mzuri wa filamu za Ghana na Nigeria utakuwa umewahi kumwona huyu binti anaitwa Juliet Ibrahim. Ana miaka 29 kwa sasa lakini ni mrembo kinoma. Binti huyo pamoja na nguli wa televisheni ya SuperSport, Robert Marawa ndiyo watakaokabidhiwa jina la staa wa Tanzania, Mbwana Samatta kwenye tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika leo Alhamisi na kumtangaza kama atashinda tuzo.
Juliet na Marawa watakuwa watangazaji kwenye shoo hiyo ya tuzo za mwanasoka bora wa Afrika zitakazofanyika mjini  Abuja, Nigeria ambayo Watanzania wengi na mashabiki wa TP Mazembe wanaisubiri kwa hamu.
Mrembo huyo ambaye ana mashabiki wengi kwenye filamu yuko fiti kwenye lugha ya Kingereza na baba yake ni Mlebanoni na Mama yake ni Mghana.
Wakuu wote wa soka duniani wakiongozwa na  Alhaji Issa Hayatou wa Fifa watazishuhudia tuzo hizo.
Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine ameongozana na Samatta anayechezea TP Mazembe ya Congo DR.  Samatta anawania tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani, huku pia akiwa Mfungaji B ora wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuifungia klabu yake ya TP Mazembe mabao manane na kuibuka mabingwa wapya wa michuano hiyo. Samatta anawania tuzo hiyo pamoja na kipa wa TP Mazembe, Robert Kidiaba na straika wa Etoile du Sahel Baghdad Boundjah ambaye ni raia wa Algeria.


Reviewed by Unknown on 01:14 Rating: 5

Hakuna maoni:

Gallery

Imetolewa na Alpha Seyongwe. Inaendeshwa na Blogger.