WASALIMIE: Benitez atimuliwa Real Madrid
Zinedine
Zidane ‘Zizou’ ataiongoza timu kwa hadi mwisho wa msimu, huku akisakwa
Kocha mpya ikielezwa Jose Mourinho ana nafasi ya kurudi klabuni hapo, baada ya
kutimuliwa Chelsea ya England.
YAMETIMIA. Kocha Rafa Benitez ametemeshwa kibarua chake,
baada ya bodi ya klabu ya Real Madrid chini ya Rais Florentino Perez kukutana
jana Jumatatu na kufikia maamuzi hayo ya kumtimua kocha huyo.Benitez
ametimuliwa ikiwa ni miezi saba tangu ateuliwa kuinoa timu hiyo Juni mwaka
jana, ikiwa ni siku moja baada ya matokeo ya sare ya mabao 2-2 dhidi ya
Valencia juzi Jumapili.
Taarifa
hizo zimedokeza kuwa nafasi yake imekabidhiwa kwa kiungo wa zamani wa timu
hiyo, Zinedine Zidane ‘Zizou’ ambaye ataiongoza timu kwa hadi mwisho wa msimu,
huku akisakwa Kocha mpya ikielezwa Jose Mourinho ana nafasi ya kurudi klabuni
hapo, baada ya kutimuliwa Chelsea ya England.
Uvumi
wa kutimuliwa kwa Benitez ulianza mapema jioni ya jana baada ya vyombo kadhaa
vya habari kudokeza kufanyika kwa kikaohicho na maamuzi yake, ingawa taarifa
rasmi iliyoka usiku mwingi kuwa, Benetez ndiyo basi tena Santiago Bernabeu.
Magazeti
mawili ya Hispania jana yaliripoti kwamba Zizou anayekinoa kikosi cha akiba cha
timu hiyo ndiye aliyekuwa akisubiriwa kutangazwa kushika nafasi ya Benitez
aliyeshindwa kupata ushindi katika mechi saba za La Liga. Na katika taarifa
hiyo ya usiku wa jana ilithibitisha kuwa ni kweli Zizzou kapewa ‘shavu’ hilo.
Benitez
aliyewahi kuzinoa Valencia, Liverpool, Napoli na Chelsea aliyokuwa kocha wa
muda, amekuwa katika kipindi kigumu tangu aliporudi Real Madrid kwa mara
nyingine baada ya kucheza soka hapo na baadaye kuwa kocha wa timu ya wachezaji
wa akiba.
Alirudi
kuchukua nafasi ya Carlo Ancelotti, Juni mwaka jana, huku habari za ndani
zilidai baadhi ya mastaa hawakuufurahia uteuzi wake.
Alijikuta
katika wakati mgumu zaidi baada ya kipigo cha mabao 4-0 ikiwa nyumbani mbele ya
Barcelona na hali kuwa mbaya Madrid ilipotolewa kwenye Kombe la Mfalme.
Reviewed by Unknown
on
07:10
Rating:

Hakuna maoni: